Saturday 5 January 2013

VIJIMAMBO: PROF JAY NA SAKATA LA KUINGIZWA MKENGE NA WAKENYA

VIJIMAMBO
thumbnail PROF JAY NA SAKATA LA KUINGIZWA MKENGE NA WAKENYA
Jan 5th 2013, 23:38

Kwa mujibu wa gazeti la The Star ka nchini Kenya, rapper Joseph Haule aka r Profesa Jay hivi karibuni aliingia kwenye mgogoro na promoter wa mjini Mombasa Kenya aliyemchukua kufanya show. Prof alikuwa amechukuliwa kufanya show mbili siku ya Christmas kwenye kumbi za Jamboree Resort na Quetu Beach Resort. 
Inavyodaiwa Profesa Jay hakuwa amelipwa fedha zote kwa show ya pili na hivyo alipewa camera aina ya Nikon D3000 kama rehani.Baada ya show, Prof aliondoka nchini Kenya na crew yake na kuibeba kamera hiyo. Sasa waandaaji hao wanadai kuwa walimpatia Prof hela yake iliyokuwa imesalia. 
Issue hiyo imekuwa kubwa kiasi ambacho passport ya mpambe aliyekuwa amesafiri na Jay nchini humo imeshikiliwa ili asiondoke.Waandaaji wanadai kuwa walimlipa Profesa Jay shilingi 252,000 za Kenya ambazo ni zaidi hata ya fedha walizokuwa wamekubaliana na sasa wanataka warudishiwe fedha yao. 
Polisi wanashughulikia kesi hiyo na Prof aliyekuwa ameingia makubaliano ya show nyingine katika ukumbi wa Jamboree December 31 aliitosa show hiyo.source na gumzo la jiji

You are receiving this email because you subscribed to this feed at blogtrottr.com.

If you no longer wish to receive these emails, you can unsubscribe from this feed, or manage all your subscriptions

No comments:

Post a Comment