Saturday 2 March 2013

VIJIMAMBO: Kondomu feki zaanza kuleta madhara Uingereza

VIJIMAMBO
thumbnail Kondomu feki zaanza kuleta madhara Uingereza
Mar 2nd 2013, 08:22

* Zaidi ya kesi 21, 000 za maambukizi mapya zimedaiwa kutambulika kwa mwaka 2011/12

WAKATI kondomu feki zilizopigwa marufuku Uingereza mwaka jana zikiwa katika mzunguko nchini Tanzania, kesi za gonjwa la ngono hatari lisilotibika zimeongezeka kwa asilimia 25 Uingereza, huku wataalamu wakionya kwamba ugonjwa huo umekuwa sugu zaidi katika tiba.

Zaidi ya kesi 21, 000 za maambukizi mapya zimedaiwa kutambulika kwa mwaka 2011/12.

Kondomu hizo feki aina ya Trojan na Durex zenye vipele vipele ambazo mwishoni mwa mwaka jana serikali ya Uingereza iliingia katika msako mkali kusaka mamilioni ya kondomu hizo bandia zilizokuwa zikiuzwa nchini humo miezi 18 iliyopita.

Kirusi kinachoambukiza ugonjwa huo hatari kimetajwa kuwa ni 'Neisseria' ambacho ni tofauti na vingine ambavyo mara nyingi hutibiwa kwa dozi moja tu ya viuavijasumu (antibiotics) ambayo angalau hufanya kazi kwa asilimia 95 kiufanisi.

Akizungumzia maendeleo ya utafiti wa kondomu hizo nchini , Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Wiwango Tanzania(TBS),Leandri Kinabo alisema shirika hilo kwa kushirikiana na Mamlaka ya Ckula na Dawa(TFDA) hivi sasa lipo katika mchakato wa kuhakikisha vipimo halisi vya ubora wa bidhaa hizo vinaangaliwa.

"Hili suala ni nyeti na ni la kiafya na usalama zaidi, hivyo tulikaa kikao na TFDA na tulikubaliana tufanye uchunguzi wa kondom hizi, kwani ni kweli zipo sokoni lakini suala la ubora linatakiwa kuangaliwa," alisema Kinabo.

Aliwataka Watanzania kuwa na subira ili waweze kuchunguza bidhaa hizo kwa umakini zaidi na kwamba baada ya uchunguzi watatoa majibu.

Baada ya gazeti hili kutaka kujua uhalali wa bidhaa hizo sokoni, Kinabo alisema bidhaa zote zinazoingia bandarini hupimwa, lakini kuna baadhi ya bidhaa ambazo huingizwa kwa njia zisizo halali na mara nyingi huwa feki.

"Inetegemea na lebo ya bidhaa husika, kuna wakati bidhaa inaweza kupimwa na kuonekana kuwa ni salama na kisha kuingizwa sokoni, lakini baada ya muda zikaingia bidhaa feki zenye nembo hiyohiyo, hivyo hilo ni suala la kusubiri vipimo kutoka TFDA," alisema Kinabo.

Tatizo hilo sugu Uingereza limesababishwa kuanzishwa kwa kampeni mpya ya kukabiliana na tishio kubwa la kuongezeka kwa kasi kwa magonjwa hayo nchini Uingereza na Wales ambayo yamedaiwa kusambaa kwa wingi nchini humo na nchi zinazoendelea.

Wataalamu wa Afya wana matumaini mapya baada ya kuanzishwa mpango mkakati wa kuzuia ugonjwa wa gono 'Gonorrhoea Resistance Action Plan' ambayo itaongeza ufahamu wa ugonjwa huo.

Mpango huo ulioanzishwa na shirika la Ulinzi wa Afya, utafuatilia tatizo hilo la kimataifa linaloongezeka kwa kasi tangu kupungua miaka 10 iliyopita.

Tatizo hili limeanza kukua kwa kasi mwaka 2011, wagonjwa wengi waliojitokeza wameugua zaidi ya mara tatu magonjwa ya ngono. Zaidi ya theluthi ya kesi hizi ni za wanaume waliokuwa wakifanya mapenzi na wanaume wenzao, kutoka karibu ya robo kwa mwaka 2010.

Profesa Cathy Ison kiongozi wa kampeni hiyo anasema "idadi kubwa ya watu waliougua magonjwa haya wanatamka kuwa walipata kutumia kondom ambazo hata hivyo baadaye zilitambulika kuwa ni feki na kuzuiwa hapa nchini Uingereza.

"Bado hatuwezi kuwahakikishia watu kuwa tunatarajia kupata suluhu ya gono hili hatari, hili bado ni tatizo kubwa kwa afya ya umma na ni kwamba sasa limeanza kusambaa hata nchi zinazoendelea," anasema Ison.

Nchini Uingereza na Wales, kuna hatari kubwa ya kuendelea kwa maambukizi haya ambayo hata hivyo yameonekana kukua kwa kasi kubwa licha ya wagonjwa wengi kudai kuwa hutumia mipira katika tendo la kujamiiana.

Ingawaje kesi za kushindwa kutibu gono hilo zimekuwa ni taarifa za kimataifa, Afisa Mganga Mkuu Uingereza, Profesa Sally Davies, hivi karibuni aliishauri serikali kuongeza nguvu katika dawa za Antibiotics kwa ajili ya dharura kwa wagonjwa watakaopatikana na gonjwa hilo.

Prof esa Davies anasema "tumeona na kuwa na wasiwasi mkubwa katika kesi za dawa sugu za magonjwa ya zinaa kwa muongo uliopita, lakini kuna haja ya kutengeneza dawa hizo kwa ajili ya tatizo hili, labda tutafanikiwa, lakini kazi ya ulinzi wa shirika la afya ni muhimu katika kutafuta suluhu ya tatizo hili" anasema.

Mdhibiti wa dawa na bidhaa za afya nchini humo, alidai kwamba mamilioni ya kondom hizo feki ziliingia nchini humo zikitokea Mashariki ya Mbali na kwamba zimeshatumiwa na watu wengi tangu kuingizwa nchini humo.

Kondom hizo zilidaiwa kutengenezwa kwa vifaa rahisi visivyo na ubora ambavyo vinaweza kuongeza hatari kwa watumiaji kwa kusambaza kwa kasi magonjwa ya zinaa, au kusababisha mimba zisizohitajika, pamoja na kuharibu mikakati ya uzazi wa mpango.(Herrieth Makwetta)
Mwananchi

You are receiving this email because you subscribed to this feed at blogtrottr.com.

If you no longer wish to receive these emails, you can unsubscribe from this feed, or manage all your subscriptions

No comments:

Post a Comment