Sunday 31 March 2013

VIJIMAMBO: NGOWI AINGIA BOTSWANA KUPROMOTI UBINGWA IBF WA KIMATAIFA

VIJIMAMBO
thumbnail NGOWI AINGIA BOTSWANA KUPROMOTI UBINGWA IBF WA KIMATAIFA
Apr 1st 2013, 00:33

FOR IMMEDIATE RELEASE – Sunday 31st, 2013- Dar-Es-Salaam - Rais wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati, Mtanzania Onesmo Ngowi amewasili katika jiji la Gaborone, Botswana kupromoti ubingwa wa IBF wa Kimataifa katika uzito wa Bantam.  
Bondia wa Botswana Lesley Sekotswe na bondia mwenzake kutoka nchini Namibia Immanuel "Prince" Naidjala walitoka sare wakati wakishindania ubingwa huo katika pambano lililofanyika katika jiji la Windhoek, Namibia tarehe 20 Mei  mwaka huu.  

Ujio wa Rais Ngowi ulikuwa unangojewa na wadau wengi wa ngumi katika nchi hii tangu aitembelee Botswana mwaka 2002 wakati wa mpambano kati ya bondia wa Botswana Thuso Kubamang na Peter Malinga kutoka nchini Afrika ya Kusini.  
Rais Ngowi atakutana na viongozi wa serikali ya Botswana pamoja na wadau mbalimbali wa ngumi na safari yake itaanzia jiji kuu la Gaborone mpaka jiji la pili kwa ukubwa la Francistown ambako wadau wengi wa ngumi wanamsubiri kwa hamu.  
Nchi ya Botswana ni nchi yenye msingi mzuri sana wa ngumi za ridhaa lakini tatizo kubwa limekuwa ni namna ya kuwaendelza wanapofikia kikomo kwenye ridhaa. Kikao cha Ngowi na viongozi wa serikali wa Botswana kitaweka msingi mzuri wa namna ya kuwaendeleza mabondia wa Botswana. 
Botswana ni nchi inayopakana na Namibia kwa hiyo mpambano wa Sekotswe na Naidjalaunategemewa kuwa na wapenzi wengi wa ngumi kutoka katika nchi hizi mbili.

Picha, Promota Kinda Nangolo wa Namibia akimwaga Rais wa IBF/Africa Onesmo Ngowi wakati akiondoka nchini humo kuelekea Botswana!

Imetolewa na :
INTERNATIONAL BOXING FEDERATION AFRICA (IBF/AFRICA)
Benjamin William Mkapa Pension Towers
Tower B, Mezzanine Floor, Azikiwe Street
Dar-Es-Salaaam


You are receiving this email because you subscribed to this feed at blogtrottr.com.

If you no longer wish to receive these emails, you can unsubscribe from this feed, or manage all your subscriptions

No comments:

Post a Comment