Wednesday 27 March 2013

VIJIMAMBO: Mwili wa mwanafunzi wa UDSM waagwa

VIJIMAMBO
Mwili wa mwanafunzi wa UDSM waagwa
Mar 28th 2013, 01:45


Naibu Makamu Mkuu wa Chuo hicho (Taaluma), Profesa Yunus Mgaya
Mwili wa aliyekuwa mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) katika Shule ya Sheria mwaka wa pili, Joseph Bernadina (25), aliyefariki juzi baada ya kujinyonga uliagwa jana katika Hospitali ya Mwananyamala, jijini Dar es salaam nakusafirishwa kuelekea Wilaya ya Ludewa mkoani Iringa kwa ajili ya maziko.


Kwa mujibu wa Naibu Makamu Mkuu wa Chuo hicho (Taaluma), Profesa Yunus Mgaya alisema mwili wa marehemu uliagwa na wanafunzi wa chuo hicho wa shule mbalimbali, Wahadhiri pamoja na wafanyakazi wa chuo na wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali.

Alisema msafara wa kuelekea Ludewa utasimamiwa na mmoja wa wafanyakazi kutoka ofisi ya Mshauri wa Wanafunzi ambaye pia atasimamia shughuli nyingine kama mwakilishi wa chuo.

Mwanafunzi huyo alijinyonga juzi kwa kutumia kamba ya manila aliyokuwa ameifunga juu ya mti katika eneo la Yombo, chuoni hapo.
 
CHANZO: NIPASHE

You are receiving this email because you subscribed to this feed at blogtrottr.com.

If you no longer wish to receive these emails, you can unsubscribe from this feed, or manage all your subscriptions

No comments:

Post a Comment